MAOMBOLEZO YA KITAIFA YA SIKU 3 KUFUATIA KIFO CHA NKURUNZINZA KUANZA LEO TANZANIA

Rais Magufuli ametangaza maombolezo ya Kitaifa ya siku 3 kuanzia leo June 13 kufuatia kifo cha Rais Nkurunziza kilichotokea June 09 Burundi,katika kipindi chote cha siku 3 za maombolezo ya Kitaifa kuanzia Jumamosi June 13 hadi Jumatatu June 15 bendera zote zitapepea nusu mlingoti.
“Burundi ni Mwanachama mwenzetu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki na Nkurunziza aliipenda Jumuiya hii, aliipenda pia Tanzania, nimeona Watanzania tuungane na Burundi katika kuomboleza na kumkumbuka Nkurunziza ambaye aliiona Tanzania kama nyumbani kwake”-JPM
#AfyayakoUPDATES

Comments